Friday, February 21, 2014

Kunywa kahawa ili Kujikinga na Saratani ya Korodani


Utafiti uliofanywa nchini Marekani umeonyesha kuwa kunywa kahawa kunaweza kusaidia kupunguza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa Saratani ya korodani ijulikanayo kanma Prostate Cancer kwa jina la kitaalam.
Uchunguzi huo umeonyesha kwamba, wanaume wanaokunywa kahawa kwa wingi hupunguza hatari hiyo kwa asilimia 60 ikilinganishwa na wanaume ambao hawanywi kahawa kabisa.

KIVIPI?
Kahawa inaathiri jinsi ambavyo mwili unayeyusha sukari, pamoja na kiasi cha homoni za jinsia, masuala ambayo yanahusiana moja kwa moja na Saratani ya korodani.
Watalamu wamesema kuwa kampaundi za kibayolojia zilizoko katika kahawa zinazuia tishu kuharibika na hivyo kupunguza uwezekano wa vimelea vya ugonjwa huo kukua kukua.
Inafaa kufahamu kwamba, Saratani ya korodani ni kensa ya pili inayowapata kwa wingi wanaume duniani na kusababisha vifo. Kati ya wanaume 6 mmoja kati yao hupatwa na saratani ya korodani.