Sunday, April 6, 2014
Mambo 5 utakayo kutana nayo katika safari ya Kufanikisha Ndoto zako
1. Utapitia wakati mgumu. Utatoka katika eneo lako la Faraja (Comfort zone).
Lakini baadaye mambo yatakaa sawa na utarudi kwenye eneo lako la faraja
2. Utaogopa.
Mara nyingine utapatwa na woga wa kufeli katika jambo unalolifanya, lakini baadaye utazoea na woga utaisha.
3. Saa nyingine utakua hauna uhakika na kile unachokifanya.
Wakati hauna uhakika unatakiwa uamue cha kufanya kati ya haya:
i. Kuachana na kile ukifanyacho na kisha kusubiria msukumo mwingine uje ukupeleke kwenye hatua inayofata. AU
ii. Kuchukua hatua ya imani na kufanya bila kujali, huku ukijua kwamba hata kama uamuzi wako utakua siyo sahihi, maisha yataendelea na utakua umejifunza kitu muhimu katika safari yako ya mafanikio.
4. Utashawishika kuacha na kujaribu kufanya kitu kingine chenye usalama/uhakika zaidi:
Usikubali kushawishika, hakuna kazi yenye usalama wa uhakika duniani kama unataka kufanikiwa.
5. Hautoweza kumfurahisha kila mtu.
Daima kutakua na watu ambao hawafurahishwi na kile unachokifanya, na kwa bahati mbaya baadhi yao wanaweza kua ni watu wa karibu yako na unao wajali. Sio tatizo; wewe funga mdoma wako na uendelee na mipango ya kufanikisha Ndoto zako bila kusubiria wakukubali. Mda sio mrefu utaanza kuona watu wanajitokeza kuungana mkono na wewe.
