Wednesday, January 8, 2014

Mwanamke ajifungua baada ya mashindano ya mbio ndefu

Amber Miller alikuwa na ujauzito wa karibu wiki 39 na alikuwa akitarajia kupata mtoto wa

pili siku yoyote wakati alipoanza kukimbia katika mashindano ya mbio ndefu (marathon) huko

Chicago, Marekani. Mwanamke huyo alikimbia na wakati mwingien akatembea licha ya

kwamba alianza kusikia misukosuko ya kiumbe kilichokuwa tumboni mwake wakati anaelekea

kumaliza mbio hizo. Hata hivyo, Miller aliweza kumaliza mbio hizo kabla ya muda mfupi

baadaye kujifungua mtoto wa kiume.

‘Mama’ huyo alimaliza mbio hizo kwa kutumia saa 6, dakika 25 na sekunde 50!